Lori laanguka na kuziba barabara muhimu Nairobi
- Saa 6 zilizopita
Msongamano mkubwa
wa magari umeshuhudiwa katika moja ya barabara kuu za kuingia jiji la
Nairobi baada ya lori kuanguka na kufuziba upande mmoja wa barabara.
Wengi
wa wakazi waliokuwa wakijiandaa kwenda kazini kutumia barabara hiyo ya
Uhuru Highway karibu wamelazimika kutumia muda mwingi kufika jijini.Ajali hiyo ilitokea usiku mita chache baada ya kupita mzunguko wa barabara wa Museum Hill ukielekea Nairobi.
Eneo hilo liko karibu na chuo kikuu cha Nairobi.
Foleni ndefu ya magari imeshuhudiwa katika barabara hiyo
Hakuna ripoti zozote za majeruhi.
Barabara hiyo hutumiwa na watu wanaotoka maeneo ya magharibi mwa jiji na pia magharibi mwa nchi kama vile Naivasha na Nakuru, Eldoret na Kisumu.


Post a Comment